Chidi mpishi

Chidi mpishi Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Chidi mpishi, Grocers, Dar es salaam, Dar es Salaam.

O African woman, love your African continent love your African heritage love your original African colorlove your origin...
22/10/2024

O African woman, love your African continent

love your African heritage

love your original African color

love your original African dress

love your beautiful african culture

LOVE AFRICA 🙏💌👍🤲?

🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹CHIDI MPISHI HAPA NAKUFUNZA KUPIKA VITUMBUA    Kuna aina nyingi ya utengenezaji wa vitumbua.  Leo napenda tuj...
15/01/2024

🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹
CHIDI MPISHI HAPA NAKUFUNZA KUPIKA VITUMBUA

Kuna aina nyingi ya utengenezaji wa vitumbua. Leo napenda tujifunze aina hii;

*Mahitaji*
🌹Mchele kilo 1
🌹Sukari 1/4kg
🌹Tui la n**i 3/4
🌹Hiliki ya unga 2tbs
🌹Hamira 2tbs
🌹Mafuta ya kupikia
🌹Unga wa mahindi 6 tbs
🌹Unga wa ngano 3 tbs.

*Matengenezo*

*K**a unatumila blenda*

🌹Loweka mchele wako masaa 6-12 na toa kwenye maji.

🌹🌹Weka kwenye blenda na saga kidogo, kisha ongeza weka hamira, hiliki na tui lako la n**i kisha saga tena,,,, mchele wako ukilainika weka Sukari na saga tena mpaka ule mchanganyiko wako ulainike,,,, baada ya hapo weka unga wa mahindi na saga kidogo kisha ongeza unga wa ngano na saga tena ili ichanganyike vizuri. Baada ya hapo weka kwenye container au bakuli na funika kwa 30dk - lisaa 1.

🌹🌹🌹 Anza kuchoma k**a ifuatavyo,,,,, weka chuma chako jikoni na acha kipate moto. Weka mafuta nusu kijiko katika kila chumba cha chuma chako,,,, Tumia upawa kuchotea na mimina kwa kila chumba. Acha kwa dk 3 na geuza upande mwingine,,,, weka tena mafuta nusu kijiko na acha kwa dk 3 tena,,,,, kitumbua chako kitakuwa tayar,,, geuza kila upande na ukiona kimekua na rangi ya udhurungi ya kupendeza kutambua chako kitakuwa tayar,,,, fanya hivyo kwa vitumbua vyote.

Hakikisha moto ni wa wastani ili usiunguze wala kubabua kitumbua chako.

*K**a hauna blenda*

Loweka mchele wako kwa masaa 3-6 na toa kisha tandaza vizuri ili ukauke

Maji yakikauka peleka kwa mashine na usage.

Weka kwa unga wa mchele kwenye bakuli kisha weka Sukari, hiliki, hamira na n**i kisha koroga vizuri mpaka ichanganyike vizuri ongeza unga wa mahindi na koroga tena kisha ongeza unga wa ngano na koroga tena.

Baada ya hapo anza kuchoma k**a nilivyoelekeza hapo juu.

🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹

Ukipenda waweza weka mayai 3 kwa huo mchanganyiko wako.

Tumia stick au kijiti kilichochongwa vizuri kugeuza vitumbua vyako,,,, pia waweza tumia spo

Hello Chidi mpishi hapa nakuelekeza kitu Katika upishi wa keki zingatia yafuatayo.Hakikisha unatumia unga wa keki sio wa...
14/01/2024

Hello Chidi mpishi hapa nakuelekeza kitu Katika upishi wa keki zingatia yafuatayo.
Hakikisha unatumia unga wa keki sio wa maandazi.(P.P.F, Azania, P.P.F self raising flour)

Tumia baking powder ya keki sio ya maandazi.(Tiara, Zesta)

Ukiona blueband ni laini Sana, punguza idadi ya mayai.

Tumia sukari nyeupe ili keki iwe Safi na muonekano mzuri ndani.

Hakikisha una measuring cups na spoons ili kupata vipimo halisi.

Ijue oven yako vizuri na usifungue oven Kila Mara ukiwa unaoka keki.

K**A BADO HAUJALIKE NA KUFOLLOW PAGE YETU HII LIKE NA KUFOLLOW SASA ILI USIPITWE NA MADARASA YANGU HAYA KWA KILA SIKU MARA TATU UKIPENDA ZAIDI JIUNGE NA GROUP LETU LA FACEBOOK KWA KUBONYEZA HAPA ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

CHIDI MPISHI HAPA NAKUFUNZA PISHI LA PILAU YA KUKU🥥🥥MAHITAJI🥥1. Mchele 1/2 kg (nusu kilo).2. Kuku mmoja wa kiasi aliyeka...
13/01/2024

CHIDI MPISHI HAPA NAKUFUNZA PISHI LA PILAU YA KUKU🥥

🥥MAHITAJI🥥

1. Mchele 1/2 kg (nusu kilo).

2. Kuku mmoja wa kiasi aliyekatwa katwa na kuoshwa vizuri.

3. Vitunguu maji 2 vilivyokatwa katwa slices.

4. Pilipili boga 1.

5. Karoti 1.

6. Dania 1.

7. Tomato/nyanya 2 zilizokatwa katwa au kublendiwa.

8. Viazi 3 vilivyokatwa katwa.

9. Tomato paste/nyanya ya mkebe vijiko 2 vya mezani.

10. Kitunguu thomu kijiko 1 cha mezani.

11. Kijiko 1 cha chai mdalasini iliopondwa.

12. Kijiko 1 cha chai pilipili manga iliopondwa.

13. Kijiko 1 cha chai bizari nyembamba iliopondwa.

14. Mafuta uto/mafuta ya kupikia takriban vijiko 3 vya mezani.

🥥JINSI YA KUANDAA🥥

➖Marinate kuku (weka s**i na chumvi kwenye kuku umuache kwa takriban nusu saa).

➖Bandika sufuria motoni ueke mafuta, yakishika moto weka kitunguu ukikaange mpaka kiwe hudhurungi (golden brown)

➖Weka spices zote(dawa za pilau) pamoja na kitunguu thomu upike kwa sekunde kadhaa
Weka tomato, pilipili boga , karoti ,tomato paste na kuku ufunike uache ziive kwa takriban dakika 10.

➖Weka mchele uupike kwa sekunde kadhaa
Weka viazi na maji kiasi. funika mpaka maji yaelekee kukauka, takriban dakika 10 (kiasi cha maji itategemea na mchele.

➖Mimi nimetumia sunrice kwa hiyo nimeweka maji kiasi cha kufunika mchele na kuzidi kidogo)
Weka dania ukoroge vizuri na uyaache maji yakauke vizuri.

➖kisha ufunike uweke moto mdogo kabisa k**a unatumia gas cooker kwa takriban dakika 10_15 (k**a unatumia jiko la makaa weka moto wa juu na chini)

Pilau ipo tayari🤗

K**A BADO HAUJALIKE NA KUFOLLOW PAGE YETU HII LIKE NA KUFOLLOW SASA ILI USIPITWE NA MADARASA YANGU HAYA KWA KILA SIKU MARA TATU UKIPENDA ZAIDI JIUNGE NA GROUP LETU LA FACEBOOK KWA KUBONYEZA HAPA ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

Kwenye maisha ya kutafuta hupaswi kuchoka wala kukata tamaa na pia hata kwenye mapenzi hupaswi kukata tamaa coz unayekup...
12/01/2024

Kwenye maisha ya kutafuta hupaswi kuchoka wala kukata tamaa na pia hata kwenye mapenzi hupaswi kukata tamaa coz unayekupenda mpende na asiyekupenda jaribu kumuacha kwa kumwambia ukweli na hata usimfiche hata awe mzuri vipi. by Chidi mpishi

CHIDI MPISHI HAPA FAHAMU JINSI YA KUPIKA MUHOGO WA KUCHEMSHA NA  JUICEJinsi yakupikaChemsha muhogo na chumvi na maji kia...
12/01/2024

CHIDI MPISHI HAPA FAHAMU JINSI YA KUPIKA MUHOGO WA KUCHEMSHA NA JUICE

Jinsi yakupika
Chemsha muhogo na chumvi na maji kiasi

JUICE
papai1 kubwa
Embe ndogo2 au hata dodo
Carot2
Tangawizi kidogo ukitaka kuona mapishi mengi zaidi ya aya basi Like page hii au NIFUATE kwenye hii page ukipenda zaidi jiunge la Group letu la Facebook kwa kubonyeza hapa ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

HELLO CHIDI MPISHI HAPA NAKUELEKEZA JINSI YA KUANDAA KUKU CHOMAViungoKitunguu swaum TangawiziVinegarSoy souceChumviOsha ...
11/01/2024

HELLO CHIDI MPISHI HAPA NAKUELEKEZA JINSI YA KUANDAA KUKU CHOMA

Viungo
Kitunguu swaum
Tangawizi
Vinegar
Soy souce
Chumvi

Osha nyama vizuri weka viungo hifadhi kwa masaa 2 choma k**a kwenye mkaa au jiko la umeme mi nimetumia oven. ukitaka kuona mapishi yangu mengine zaidi ya aya basi Like hii page au NIFUATE kwenye hiii page yangu ukipenda zaidi jiunge na Group letu la Facebook kwa kubonyeza hapa ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

CHIDI MPISHI HAPA LEO NAWAELEKEZA JINSI YA KUTENGENEZA KINYWAJI CHA JUICE TENA JUICE YA EMBEmahitajiEmbe 4Passion 1Maji ...
11/01/2024

CHIDI MPISHI HAPA LEO NAWAELEKEZA JINSI YA KUTENGENEZA KINYWAJI CHA JUICE TENA JUICE YA EMBE
mahitaji
Embe 4
Passion 1
Maji Lita 2
Sukari vjko 3
Tangawizi kipande kidogo

Osha ba menya vitu vyote weka kwenye blender saga mpaka iwe laini kisha chuja na tayari kwa kunywewa. K**a maji hayakuwa baridi weka kwa fridge 30mn.😋😋 ukitaka kuona mapishi yangu mengi zaidi basi Like Page hii au NIFUATE kwenye hii page ukipenda zaidi jiunge na Group letu La kwenye Facebook kwa kubonyeza hapa ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

Mtu Maskini na TajiriTajiri: Wewe mpumbavu Njoo hapaMtu mas**ini: Mimi ?Tajiri: Ndio ni nani mwingine unamuona kando yak...
09/01/2024

Mtu Maskini na Tajiri
Tajiri: Wewe mpumbavu Njoo hapa
Mtu mas**ini: Mimi ?
Tajiri: Ndio ni nani mwingine unamuona kando yako,
Mtu mas**ini: sawa NIAMBIE,
Tajiri: unataka nini maishani?
Mtu mas**ini: Namtaka Mungu katika Maisha
yangu,
Tajiri: Mungu ni nani?
Mtu mas**ini: Yule aliyekupa vitu vyote
Ulivyonavyo
Tajiri: Je! Anakujali ??
Mtu mas**ini: Ndio ananijali sana,
Tajiri: hahahahaha
Mtu mas**ini: Nini kikichekesheshasho??
Tajiri: Hebu jiangalie.
Mtu mas**ini: Ninajivunia hivi nilivyo maana
Mungu ananipenda,
Tajiri :: Vipi kuhusu huyu anayesoma hii!
Je! Mungu huwajali?
Mtu mas**ini :: ndiyo Mungu huwajali
HEBU TUONE
MUNGU: Leo nimemic mtu huyu anaesoma
maandiko yangu,.
SHETANI: Mtu!!!! Mtu gani hahhahaa,
MUNGU: Huyu anaetabasamu, na kusema shetani
huwa kila siku yeye mbishi,.
SHETANI: Hahaha hapana Ila wewe huwa
unawatetea tu, kila siku nakuambia hakuna mtu
yoyote anaependa kusoma mafundisho yako,
nasema hivyo maana nawaeleza vizuri, # kusoma tu
yenyewe hapa, kashachoka,.
MUNGU: Usinidanganye na usijidanganye sasa kaa
ukijua kuwa leo unaenda kuaaibika maana maneno
haya yatasabaswa mpaka VIBARAKA vyako
vitasoma, na kila mkono utakaoshare na kusema,
AMEN, NTAAMBATANA NA NDOTO ZAKE
BARABARA, MPAKA NIHAKIKISHE AMEFANIKIWA
K**A ALIVYONISAIDIA KUFANIKISHA NENO HILI
LITAPAKAE KOTE DUNIANI ,.
SHETANI, Mimi huwa si mbishi, tutizame jinsi
unavyoenda kupuuziwa na watu wako na neno lako
wala hawajalisoma , na wala hawatasambaza hii
MWANA WA MUNGU SAMBAZA UJUMBE HUU UWEZAVYO HADI SHETANI ASHANGAE..🙏🙏

HELLO CHIDI MPISHI HAPA NAKUELEKEZA JINSI YA KUANDAA NA KUPIKA BAGIA NYUMBANI.VipimoKunde  za kupaaza - 1 ½  VikombeVitu...
08/01/2024

HELLO CHIDI MPISHI HAPA NAKUELEKEZA JINSI YA KUANDAA NA KUPIKA BAGIA NYUMBANI.

Vipimo

Kunde za kupaaza - 1 ½ Vikombe

Vitungu vya kijani iliyokatwa katwa - ½ Kikombe

Baking soda - ¼ Kijiko cha chai

*Bizari mchanganyiko - 1 Kijiko cha chai

Maziwa - 2 Vijiko vya supu

Chumvi - 1 ¼ Vijiko vya chai

Unga wa ngano - 2 Vijiko vya supu

Mafuta ya kukaangia

* Unaweza kutumia bizari ya pilau (cu**in) ukipenda

Namna ya kutayarisha na kupika

Osha na kuroweka kunde kwenye bakuli la maji ya baridi usiku mpaka asubuhi.Saga kwenye mashine (food processor) kisha mimina kwenye bakuli.Ongeza vitungu, baking soda, masala, maziwa, na chumvi.Koroga vizuri halafu tia unga kisha uchanganye pamoja.Fanya vidonge k**a nchi moja kisha ukipenda bana katikati ya mikono na kidole katikati ya bajia.Kaanga kwenye mafuta ya moto mpaka ziive.Andaa bajia kwenye sahani na chatini uipendayo. ukitaka kuona mapishi mengine zaidi ya aya basi Like page hii au NIFUATE kwenye hii page yangu ukipenda zaidi jiunge na Group letu kwa kubonyeza hapa ➡️ https://facebook.com/groups/177482772873123/

Habari mimi ni kijana wa miaka 37, nilioa lakini kwa bahati mbaya niliachana na mke wangu, alikua ni mbinafsi sana hapen...
07/01/2024

Habari mimi ni kijana wa miaka 37, nilioa lakini kwa bahati mbaya niliachana na mke wangu, alikua ni mbinafsi sana hapendi ndugu zangu hivyo nikaamua kuachana naye, nilikua na watoto wawili nikawachukua naishi nao kwa Kaka yangu. nina Kaka yangu ni mfanyakazi wa tyaasisi flani kubwa tu na ana kipato kikubwa, mimi nafanya kazi na mshaara wangu ni k**a laki tano hivi hivyo sijaweza kujitegemea kwa kuwa na nyumba yangu.

Naishi kwa Kaka yangu ambaye naye kaoa ana watoto wanne, mkubwa ana miaka 19. Shida inakuja hivi, hapa kwa Kaka mke wake ni Mama wa nyumbani, kasoma lakini hataki kufanya kazi kajikalia tu anasimamia bisahara za Kaka. Shid ainakuja katika mali za Kaka, kaka anamuamini sana mke wake kuliko hata sisi ndugu zake, yaani kuna kipindi shemeji anandiaharau, watoto wake wanatukana watoto wangu lakini Kaka ukimuambia anapuuzia.

Hilo si shida kwani huyu mwanamke hakuna mtu hata mmoja ambaye anampenda ndugu wote hawtaaki hata kuja kwasababu ya roho mbaya yake mimi kwakua nampend Akaka yangu basi nimeamua kuja kuishi hapa. Shid inakuja kuwa, huyu mwanamke ndiyo ananunua kila kitu na kibaya nikuwa kila kitu kaandika majina ya watoto.

Yaani mali zote, kuanzia viwanja mpaka makampuni ya Kaka mwanamke kamshawishi kaandika watoto. Kibaya aidi nikuwa watoto wapo upande wa Mama yao, shemeji kawajaza maneno mpaka wanatuchukia sisi hivyo hata ikitokea mfano kwa bahati mbaya kaka akifariki kwakua kila mtu kaumbiwa mauti, mali zote za kaka zitakua za wanae na kwakua wanampenda Mama yao basi zitakua ni za mwanamke, sisi tutapata nini wakati ndiyo ndugu zake wa damu. Naomba nisaidie kisheria hapa inakuaje kwani naona k**a sisi tunadhulumiwa mali!

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chidi mpishi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category