14/08/2023
FAHAMU JINSI YA KUSOMA MATAIRI
Ulishawai kuangalia pembeni mwa tairi na kukuta kuna herufi na namba na ukatamani kujua nini maana yake. Nimewaletea ishara na alama ambazo huwekwa kwenye tairi ili kila dereva ajue nini maana zake.
Alama ambazo huwekwa kwenye tairi huelezea;
1. Ukubwa wa tairi.
Baadhi huwekewa maeleze kuhusu ukubwa wa tairi na ni maelezo muhimu sana kuwepo kwenye tairi. Kila namba na kipengele inakua na maana tofautitofauti kwenye tairi. Inaonekana k**a hivi;
165/65/R14 79 T.
• 165 - Upana wa tairi kwa milimita
• 65 - Urefu wa tairi kutoka chini kwenda juu kwa asili demia. Mfano, ni asilimia 65 ya upana wa tairi.
• R - inamaanisha kipenyo cha tairi yaani Radius kwa lugha ya wenzetu
• 14 - Inamaanisha ukubwa wa rim kwa kipimo cha inchi.
• 90 - 90 code ya uzito wa kubeba
• V - Inamaanisha speed/Kasi.
Herufi “V” yenyewe ipo hapa kwa mfano na inaweza ikawa herufi yeyote k**a vile “H”, “L”, “M”, “N” “O” “P” “Q” “R” “S” “T” “U” “V” “W” “Y”“W”.
Herufi hizi zinawakilisha mwendo kasi unaoruhusiwa na matairi haya. Na ili uweze kuzielewa zipo indices ambazo zinatambulika kimataifa k**a tafsiri sahihi ya mafumbo-namba haya.
Mafumbo ya mzigo kiasi gani unaruhusiwa kwa tairi yako;
62…… inaruhusiwa kubeba hadi Kg 265
75…… inaruhusiwa kubeba hadi Kg 387
88…….inaruhusiwa kubeba hadi Kg 560
101…...inaruhusiwa kubeba hadi Kg 825
114……inaruhusiwa kubeba hadi Kg 1180
63….....inaruhusiwa kubeba hadi Kg 272
76….....inaruhusiwa kubeba hadi Kg 400
89….....inaruhusiwa kubeba hadi Kg 580
102…...inaruhusiwa kubeba hadi Kg 850
115…...inaruhusiwa kubeba hadi Kg 1215
64…….inaruhusiwa kubeba hadi Kg 280
77…….inaruhusiwa kubeba hadi Kg 412
90…….inaruhusiwa kubeba hadi Kg 600
103…...inaruhusiwa kubeba hadi Kg 875
Hivyo k**a gari yako ina namba 62 ambayo inaruhusu kubeba hadi 265Kg tu huwezi kubeba mzigo wenye uzito wa 600Kg ambao tairi yenye nambari 90 ndiyo inayomudu au yenye nambari ya juu Zaidi.
Mafumbo namba ya mwendo kasi na maana yake ni k**a yafuatayo:
L…..inaruhusu hadi 120 Km/h.
M…..inaruhusu hadi 130 Km/h
N…..inaruhusu hadi 140 Km/h
P…..inaruhusu hadi 150 Km/h
Q…..inaruhusu hadi 160 Km/h
R…..inaruhusu hadi 170 Km/h
S…..inaruhusu hadi 180 Km/h
T…..inaruhusu hadi 190 Km/h
U…..inaruhusu hadi 200 Km/h
H…..inaruhusu hadi 210 Km/h
V…..inaruhusu hadi 240 Km/h
W…..inaruhusu hadi 270 Km/h
Y…..inaruhusu hadi 300 Km/h
Hivyo ikiwa tairi yako ina namba L inayokuruhusu spidi hadi 120 na si Zaidi, jua hauwezi kuendesha kwa spidi 150 ambayo ni kwa ajili ya nambari “P” au ya Zaidi yake.
2. Kuonesha uelekeo.
Sio matairi yote huonesha uelekeo, ni muhimu kujua ni sehemu gani au upende gani wa tairi unatakiwa kuzunguka. Yaana namaanisha ni upende gani utakiwa kukaa nje na upende gani kukaa ndani. Pia Kuna matairi huwekwa direction ya tairi kuzungukia.
3. Kiwango kikubwa cha mizigo na shinikizo.
Matairi yana kiwango cha mwisho cha kubeba mizigo pamoja na shinikizo(pressure). Kitabu chako kitakuonesha ni kiwango gari inatakiwa ibebe ambayo ni sahihi kwa uendeshaji wako wa kilasiku.
4. Kiashiria cha tairi kuisha.
Baadhi ya watengenezaji wa matairi huweka kikomo cha kukanyaga au kuisha kwa matairi. Kikomo hichi kimewekwa pindi tairi lako likiisha na kufikia 1.6 milimita unahitaji kubadilisha tairi. Hapa kibongobongo tunasema tairi linakipara.
Mengine ni k**a brand ya tairi, nchi lilipotengenezewa, material na pattern.
Pia matairi yanaelezea mwaka yalipotengenezwa.
Ukiangalia kwenye picha chini kuna namba nne za mwisho ambazo ni hizo 1309:
13 - inamaanisha wiki ya tairi kutengenezwa.
09 - inamaanisha mwaka wa kutengenezwa
Kwaio tairi limetengenezwa wiki ya 13 mwaka 2009.
Usisite kutufollow kwenye kurasa yetu Mycar Tanzania like, comment na share ili uwe wa kwanza kupata update.