lukawandeto65gmail.com

lukawandeto65gmail.com Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from lukawandeto65gmail.com, Grocers, Karen.

23/12/2025

Zaburi 49
4 Nitatega sikio langu nisikie mithali, Na kufumbua fumbo langu kwa kinubi

5 Kwa nini niogope siku za uovu, Ubaya ukinizunguka miguuni pangu?

6 Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao;

7 Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,

15 Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu, Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanikaribisha.

17 Maana atakapokufa hatachukua cho chote; Utukufu wake hautashuka ukimfuata.

18 Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, Na watu watakusifu ukijitendea mema,

20 Mwanadamu mwenye heshima, iwapo hana akili, Amefanana na wanyama wapoteao.

28/08/2025

Yeremia 30:17
Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye.

13/05/2025

489.4K likes, 6836 comments. “Good morning Jesus.”

09/01/2025

Waebrania 12
18 Maana hamkufikilia mlima uwezao kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani,

19 na mlio wa baragumu na sauti ya maneno; ambayo wale walioisikia walisihi wasiambiwe neno lo lote lingine;

20 maana hawakuweza kustahimili neno lile lililoamriwa, Hata mnyama akiugusa huo mlima atapigwa kwa mawe.

22 Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,

23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,

24 na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.

25 Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni;

26 ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia.

27 Lakini neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa, k**a vitu vilivyoumbwa, vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae.

28 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;

29 maana Mungu wetu ni moto ulao.

09/01/2025

1 Petro 4
1 Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.

2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.

5 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

6 Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili k**a wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho k**a Mungu alivyo hai.

7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.

8 Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

9 Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika;

10 kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; k**a mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.

11 Mtu akisema, na aseme k**a mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata k**a moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

13 Lakini k**a mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

15 Maana mtu wa kwenu asiteswe k**a mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au k**a mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?

18 Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?

19 Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, k**a kwa Muumba mwaminifu.

27/07/2024

Yeremia 1
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.

7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.

8 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.

9 Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;

10 angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.

11 Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi.

12 Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.

23/07/2024

Zaburi 118
14 Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.

15 Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.

16 Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.

17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.

18 Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.

19 Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.

20 Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.

21 Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.

22 Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

23 Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.

22/07/2024

Kumbukumbu la Torati 30
10 ukiwa utaifuata sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa kuyashika maagizo yake, na amri zake zilizoandikwa katika chuo hiki cha torati; ukimwelekea Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote.

11 Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.

12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?

13 Wala si ng'ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?

14 Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;

16 kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda Bwana, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki.

17 Lakini moyo wako ukikengeuka, usipotaka kusikiza, lakini ukavutwa kando kwenda kuabudu miungu mingine, na kuitumikia;

18 nawahubiri hivi leo hakika mtaangamia; hamtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi, uivukiayo Yordani, uingie kuimiliki.

21/07/2024

6824 likes, 120 comments. “ 🔥🔥🔥 🔥🔥🔥 ”

21/07/2024

37.3K likes, 450 comments. Check out Blessings’s video.

Address

Karen

Telephone

+254728396564

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when lukawandeto65gmail.com posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to lukawandeto65gmail.com:

Share

Category