19/03/2026
🗣️🎙️Paul Pogba:
“Wakati mwingine watoto wangu hulalamika wakiwa hapa Ulaya. Nawaambia: ‘Nitawapeleka tena Afrika ili muone maisha ya shida yalivyo.’
Mimi nilikulia kwenye maisha ya uhaba, si maisha ya kutafuta visingizio. Nilijifunza kupambana na kujituma, si kusubiri mafanikio yaje yenyewe. Hiyo ndiyo ilinifanya nifikie kuwa mchezaji mkubwa wa soka.
Hicho ndicho ninachotaka watoto wangu wajifunze: wasichanganye maisha ya raha na kudhani kila kitu ni haki yao.
Sijali k**a watachagua soka, muziki au kipaji kingine chochote wanachokipenda. Kitu ninachotaka tu ni wawe na hamu ya mafanikio — hamu ya kukua, kujituma na kuwa na shukrani.
Nyumbani kwangu, chakula lazima kimalizwe kwenye sahani. Kila mara. Kwa sababu najua maana ya kulala njaa.
Sitaki watoto wangu wawe tu matajiri. Nataka wawe watoto wanaojua thamani ya maisha, hata k**a wanaishi kwenye mazingira ya neema na fursa nyingi.”