20/04/2026
Wanaharakati wengi Wa Zanzibar wanaoitaka Zanzibar yao ijitenge na Tanganyika, wanatakiwa kujua endapo Tanzania Bara itajitenga nao, basi watakuwa gizani daima kwa sababu umeme wote unaowaka huko unatokea Bara.
Na mbaya zaidi visiwa hivyo havina ukaribu wa kijiografia na nchi nyingine za karibu zinazoweza kuwapa umeme zaidi ya Tanzania Bara.
Kwa kutumia cable za chini ya maji, umeme wenye Kilovoti 132 unatokea Ras Kiromoni (Dar es Salaam) hadi Mtoni (Zanzibar).
K**a hiyo haitoshi umeme mwingine wa Kilovoti 33 unatokea Tanga - Majani Mapana hadi Pemba- Ras Mkumbuu maana yake basi visiwa vyote hivyo vinawashwa taa, vinachaji simu, vinaendesha viwanda kwa umeme wa Bara.
Je, Watakachokosa wa Tanzania Bara kutoka Zanzibar ni kipi hasa cha kuwasikitisha?