24/03/2023
USITAFUTE PESA ILI UPATE VITU,TAFUTA VITU UPATE PESA.
Makala hii itakuchanganya kidogo msomaji wangu lakini piga moyo konde utaelewa tu.
Pesa hutafutwa na maskini ila vitu hutafutwa na matajiri.
Kuna vitu ambavyo pesa haiwezi kununua.
Ila vitu vinaweza kuleta Kila aina ya pesa.
Ndiyo maana ukisikia tajiri amekufa,hawahesabu pesa alizoacha Bali vitu alivyoacha.
Hapa sizungumzii vitu K**a magari,la hasha .
Nazungumzia rasili Mali.
Yaani mashamba,mifugo,madini ,ardhi,mafuta nk.
Ngoja nikufute wasiwasi,vitu K**a hivyo vinaweza kuleta pesa kwa muda mfupi Sana na ukaanza kuhesabu noti za kutosha.
Lakini ukianza kutafuta noti,njia yake nyepesi ni Wewe kuajiriwa.
Sasa mfano,kwa mwezi unalipwa 500$,ukikata na gharama za matumizi zinabaki 300$,
Sasa ukipiga hesabu kwa mwaka utakuwa una hifadhi ngapi???
300×12.ni sawa na Dola 3600 kwa mwaka.
Pesa ambazo hazijatosha hata kwa kununua gari la kumpeleka mtoto wa jirani yako shule.
Je lini utatoka kwenye umaskini????
Sasa mwenzako wa vitu,alinunua nguruwe SITA,dume mmoja,dike watano. Baada ya kukomaa hawa wanazaa Kila mmoja nguruwe Saba. Na wakilizhwa vizuri anawatoa Kila baada ya miezi SITA. Kwa bei ya Dola 300$.
Sasa kwa mwaka anaingiza ngapi ikiwa baada ya miezi SITA anauza nguruwe 20???
Elfu SITA hiyo kirahisi tu,
Ni mfano nimetoa.
Siyo hapo tu,
Unaweza ukakumbuka malkia Elisabeth wa Uingereza alipokufa,ni kipi kilioneshwa K**a hazina alizoacha???
Yalikuwa madini yasiyo na hesabu,yaani Almasi,dhahabu,Shaba,nk.
Unajua sasa hivi waaabu ni matajiri Sana na ni kipi kinawapa utundu????
Kwanza wanamiliki hazina ya mafuta iliyo kubwa kuliko zote duniani,na ni wazalishaji wa matunda kuliko wengine duniani.
Hiyo yote ni Nini????
Wanamiliki vitu na si pesa.
Ukisikia mtu anakuambiya utafute pesa hataki uwe tajiri kwa sababu utatumikishwa ili uzipate pesa.
Ulishawahi kuona tajiri ameajiriwa???
Kutafuta pesa ni kuwa mtumwa wa pesa lakini ukitafuta vitu unakuwa boss wa pesa.
Siri za Dunia.