04/02/2025
VIDONDA VYA TUMBO
*Je, vidonda vya tumbo ni nini?*
Vidonda husababishwa na kubanduka kwa utando ambako hutokea wakati ambapo sehemu ya nyama wa tumbo au utumbo zimeharibiwa.
"Ukuta wa tumbo na duodenum ni pamoja na tabaka nne na mgonjwa husemekana kuwa na ugonjwa wa vidonda/ kidonda cha tumbo wakati kidonda kinapofikia safu ya tatu."
*Je! ni kidonda/vidonda vya tumbo husababishwa na nini?*
Chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo ni bakteria Helicobacter pylori (H. pylori) wanaopatikana katika asilimia 90 ya matukio na matumizi ya dawa za kuzuia maumivu zisizo na steroide (NSAIDs).
“Tunapozungumzia sababu za vidonda tutatofautisha aina mbili , kwanza ni maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori, ni bakteria ambao tunawapata tukiwa wadogo kwa kula vitu mbali mbali ambão husababisha uzalishaji mwingi wa asidi tumboni ambayo inaweza kusababisha kidonda,”
Sababu ya pili ya vidonda ni tabia fulani na mambo ya maisha, ambayo yanaweza kuchangia kuongezeka kwa bakteria hawa au kuzidisha vidonda vilivyopo.
"Ni ukweli, kwa mfano, kufunga, kuruka mlo, au kutumia dawa zenye asterods uchochezi, hususan aspirini au ibuprofen."
Sababu nyingine ni matumizi ya "pombe kwenye tumbo tupu. Kwa hivyo vitu hivi vitagusana moja kwa moja na utando wa tumbo au ule wa sehemu ya mwisho ya tumbo inayosafirisha chakula kwenye utumbo na kusababisha uvimbe ambao unaweza kusababisha kidonda,"
TABIA ZINAZOWEZA KUONGEZA UWEZEKANO WA KUPATA VIDONDA VYA TUMBO.
1. Uvutaji sigara
2. Unywaji pombe kupita kiasi
3. Msongo wa mawazo
4. Unywaji wa kafeini kupita kiasi
5. Kula kupita kiasi
6. Kupuuza Dalili za Vidonda
7. Matumizi kupita kiasi ya Antacids
*DALILI ZAKE NI ZIPI?*
Vidonda vya tumbo hujidhihirisha kwa maumivu ya epigastric: epigastrium ni kiungo kilichopo katikati ya juu ya tumbo.
Mgonjwa huhisi hali ya kuungua kukandamizwa kwenye tumbo la juu. Maumivu haya huwa makali sana katika saa za kwanza baada ya kula na hupungua unaposhiba.
Ugonjwa huo pia unajidhihirisha na dyspepsia, yaani, hisia ya uzito wa tumbo, tumbo kushindwa kumeng’enya chakula k**a kawaida, kichefuchefu au kutapika au katika hali mbaya zaidi kwa kutokwa na damu.
Njoo ujipatie dawa za vidonda vya tumbo 0743343483