ATJAM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ATJAM, Grocers, Goba Mpakani, Dar es Salaam.

28/04/2026

NENO LA SIKU

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha

Tarehe: 28/04/2026

SOMO: NENO LA MUNGU LIKIKOSEKANA NDANI YAKO NI RAHISI KUMKOSEA MUNGU

Zaburi119: 11 "Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako, nisije nikakutenda dhambi"

Wewe uliyemwana wa Mungu unapaswa kuliweka Neno la Mungu moyoni mwako ili uwe salama. Haiwezekani umuombe Mungu juu ya kupata mtaji wa biashara yako halafu shetani aje kuchezea biashara yako mpaka inakufa.

Wewe uliye na Neno la Mungu ndani yako haiwezekani shetani aje achezee ndoa yako mpaka ivunjike, ukiona hivyo tambua kuwa kuna mahali hautendi sawa sawa; kwa maana Kristo akiwa ndani yako inamaana kuwa Nuru ipo ndani yako hivyo giza haliwezi kukaa kwako.

K**a Neno halipo ndani yako ni rahisi kumtenda Mungu dhambi. Neno haliwezi kukaa kwako k**a Yesu hayupo ndani yako kwa sababu Yesu na Neno ni mmoja. Yesu akiwa ndani yako maana yake Neno lipo ndani yako na Neno likiwa ndani yako wewe utazaa matunda.

Sauli alimkosea Nabii wa Bwana Samweli mara mbili kwa kukosa adabu matokeo yake akaangamizwa. Kuna watu wengine wanasema wameokoka lakini wanakosa adabu mbele za Mungu, hawamuheshimu Mungu tena kwa maana wanawadharau Watumishi wa Mungu.

Usipokuwa na adabu na kuwa mtii kwa Mtumishi aliyepakwa mafuta na Mungu na kuwekwa mbele yako ili kukuongoza basi huyo Mtumishi anao uwezo mkubwa wa kukuondolea talanta yako, nafasi yako na baraka zako.

Mungu akusaidie kuelewa hii siri uweze kufikia malengo ya kuumbwa kwako. Natamani wanangu mfike mahali pa kushangilia baraka zenu; lakini k**a utakuwa siyo mtii na utakosa adabu utamfanya Mungu asisikie maombi yako.

20/04/2026
20/03/2026

NENO LA SIKU

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha

TAREHE: 20/03/2026

SOMO: NGUVU YA MAWAZO

Mwanzo 6:5-6 “Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.”

Maisha ya mtu yanaweza kuathiri wengine kwa kiasi kikubwa. Mawazo mabaya yanaweza kusababisha maangamizi kwa watu, vitu na hata mazingira yanayomzunguka mtu. Hivyo, kile unachowaza kina mchango mkubwa katika matokeo ya maisha yako na ya wengine.

Sisi ambao tumeitwa kwa jina lake lazima tulichunguze hilo, Je! umekuwa wa namna gani katika maisha yako? Je! unachangia maangamizi au unachangangia uponyaji? Jamii unayoizunguka inaponyeka au inateseka.

Lakini Mungu, kwa upendo wake alimtuma Yesu Kristo kuleta ukombozi na uponyaji. Alituwazia mema ili atuondoe kwenye mawazo mabaya. Hivyo basi, nasi tunapaswa kubadilika na kuwaza mema k**a Mungu anavyowaza, ili tuwe chanzo cha baraka kwa wengine.

19/03/2026
06/03/2026

NAIBARIKI IJUMAA YANGU.

Kwa maana nimefunguliwa Mlango Mkubwa wa kufaa sana; Mimi ni Hodari, Mimi nina Moyo wa Ushujaa, Mimi ni Mshindi, maana BWANA amenipa kushinda.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

05/03/2026

Unapokaribia baraka, maadui nao huinuka.

Lakini kumbuka — upinzani si ishara ya kushindwa, bali ni uthibitisho kwamba uko karibu kumiliki kilicho chako.

.

'swill

05/03/2026

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.

Kwa maana nimefunguliwa Mlango Mkubwa wa kufaa sana; Kwangu hakutapungua Kicheko, Sherehe, Furaha, Tafrija, Karamu na Utele.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

Address

Goba Mpakani
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ATJAM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category